Wakenya Wamchangia kwa Ukarimu Babake Albert Ojwang, Wateta M-Pesa Yake Imejaa

Wakenya kutoka tabaka mbalimbali wamejitokeza kumuonyesha babake marehemu bloga Albert Ojwang kwamba hayuko peke yake na kwamba yupo katika mawazo yao kupitia michango ya pesa taslimu na M-Pesa

Wakenya walianza kumhurumia mwanaume huyo wa makamo baada ya kuvunjika moyo akitangaza kifo cha mwanawe, na M-Pesa yake ikajaa ndani ya dakika 11 tu baada ya tangazo hilo

Walilazimika kutafuta nambari nyingine ya kusaidia kuchangisha, na Wakenya wakaapa kuijaza pia. Eric Omondi aliwaomba watumie Pochi La Bishara iwapo nambari hiyo mpya itajaa pia

Nairobi, Kenya: Wakenya wenye ukarimu wamejitokeza kwa wingi kumshika mkono Meshack Opiyo kwa michango ya hali na mali, kufuatia kifo cha kikatili cha mwanawe wa pekee, Albert Ojwang.

Mchekeshaji Eric Omondi akimfariji Meshack Opiyo (kshoto), marehemu Albert Ojwang.

Chanzo: Facebook

Meshack alionekana kwa mara ya kwanza kwenye vyombo vya habari akiwa amevunjika moyo baada ya kufahamishwa kuwa mwanawe, ambaye alikuwa amesafiri kumwokoa, alikuwa tayari amekufa.

Mnamo Machi 10, matokeo ya uchunguzi wa maiti yalitolewa na ikaonekana wazi kuwa kijana huyo aliuawa kwa kupigwa na polisi akiwa ndani ya seli.

Uthibitisho huu kuhusu chanzo cha kifo chake uliwaacha Wakenya wengi wakiwa na hasira kali, wakazua maandamano mitaani hadi Jogoo House na pia kwenye mitandao ya kijamii.

Wengi walikuwa wakitafuta nambari yake ya simu ili kumtumia pesa za kusaidia kwa maandalizi ya mazishi na pia kumfariji kwamba wanamwombea.

Hatimaye waliipata baada ya mchekeshaji Eric Omondi kuthibitisha nambari hiyo.

?Jamani watu wangu Mungu awabariki kwa msaada mkubwa sana... ujumbe wa M-Pesa umejaa. Hii hapa ni nambari nyingine ya babake Albert Ojwang' ? 0113664965 (Meshack Opiyo). Tuendelee kutuma. Unaweza pia kutumia pochi la biashara kwenye nambari hii nyingine 0727927898 (Meshack Opiyo). Mungu awabariki,? alisema Omondi.

?Ndani ya dakika 11 tu baada ya kuposti nambari ya Meshack, tayari imejaa. Tumeweza kupata nambari nyingine, nayo pia inasoma Meshack. Amenipigia na kuniambia ?Eric tafadhali waambie Wakenya asanteni sana,?? aliongeza.

Albert Ojwang wakati wa furaha zaidi. Picha: Danish Odongo.

Chanzo: Twitter

Maoni ya Wakenya yalimaanisha nini?

Kulingana na mtumiaji wa Facebook aliyejitambulisha kama Isaac Kimtai, nambari ya M-Pesa ya baba yake Albert kujaa ndani ya dakika 33 haikuwa tu mchango wa kawaida bali tukio kubwa la kitaifa.

?Ndiyo, ni huruma lakini pia ni kilio cha hasira. Ni majonzi ya pamoja, ni uasi wa kidijitali,? alisema katika video ya Facebook.

?Albert si jina tu. Ni mwathiriwa wa ukatili wa polisi, kijana mwingine wa Kenya aliyezimwa na mfumo uliopaswa kumlinda. Na Wakenya hawageuki macho upande mwingine. Wanaonyesha mshikamano kwa simu zao, sauti zao, na pesa zao kwa sababu wamechoka. Wamechoka na ukosefu wa haki. Wamechoka na kimya. Wamechoka kuona ndugu na dada zao wakifa bila mtu kuwajibika.?

Akizungumza na TUKO.co.ke, wakili Collins Wanderi, ambaye pia alishiriki katika mchango huo, alisema kuwa Pochi ilikuwa inafanya kazi vizuri kabisa.

Collins Wanderi:

?Ero kamano ahinya wuod minwa. Pochi inafanya kazi vizuri kabisa. Mzee Opiyo amepokea kitu kutoka kwenye mioyo yetu. Pole nyingi kwake, mkewe, mjane na mtoto aliyeachwa na Albert. Mwambie Mzee Opiyo hatatembea peke yake kamwe.?

Wakenya watoa maoni yao kuhusu habari hizo:

Mu Ga:

?Great work Eric. Itabidi uwasiliane na Safaricom PLC waweze kufungua Paybill au till ya muda. Hata hiyo nyingine itajaa hivi karibuni.?

Jesca Kiplagat:

?Hii ni Jesca Kiplagat.. Nimeshare post yako kuhusu Baba Albert.. Tafadhali mwambie M-Pesa yake imejaa.?

Lucy Ndunguh:

?Kazi nzuri Eric.....si hata kifedha tu, kama unaweza kumtembelea yule mzee kimwili, umshike bega anapovunjika, umwombee sala hiyo ni msaada mkubwa pia maana kifo cha mwanawe najua kinamvunja sana kiakili.?

Hon. Opiyo Oswago:

?Mimi sasa nimeshalia, macho zinataka kutoka Eric Omondi. Space kidogo nitatafuta nayo nitume! Wacha tutume hii pia ijae...Wakati huo huo, tunaomba kikao na Langat. Kila mtu lazima aende.?

Albert Ojwang' aelekeza matumaini kwa William Ruto

Awali, Meshack Opiyo aliamini kuwa polisi waliomkamata mwanawe walimuua kwa sababu waliona familia yao ni ya kipato cha chini.

Baadaye alizungumza na Rais William Ruto na kuomba msaada kwa kuwa yeye pia ni mlia ushuru wa hadhi ya chini.

Wanasiasa, raia wa kawaida, na marafiki wamelaani kwa kauli moja mauaji haya ya kikatili.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke