Albert Ojwang: CCTV Yaonyesha Askari Hawakuwa na Haraka baada ya Kuuleta Mwili wa Bloga Hospitalini

Maafisa wa polisi waliousafirisha mwili wa Albert Ojwang' kutoka Kituo Kikuu cha Polisi hadi Hospitali ya Mbagathi walionekana wenye wasiwasi

Kamera za CCTV zilinasa maafisa hao wakizungumza kwa simu na watu wasiojulikana kwa muda kabla ya kumuondoa Ojwang' kwenye gari na kumuingiza hospitalini kwenye kitanda cha machela

Madaktari wa zamu katika Hospitali ya Kaunti ya Mbagathi walithibitisha kuwa Ojwang' aliaga dunia, kwa kuwa moyo wake ulikuwa haupigi

Nairobi - Picha za kipekee za CCTV katika Hospitali ya Kaunti ya Mbagathi zimeleta mtazamo mpya kuhusu hali ya mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang'.

Albert Ojwang aliuawa akiwa katika seli katika Kituo Kikuu cha Polisi, Nairobi. Picha: Alberto Januzaj.

Chanzo: Twitter

Mwanablogu huyo aliuawa muda mfupi baada ya kuzuiliwa peke yake kwenye seli katika Kituo cha Polisi cha Central, Nairobi, saa chache baada ya kutolewa nyumbani kwao Homa Bay.

Baada ya kuteswa hadi kufa, polisi waliuweka mwili wa Ojwang' nyuma ya gari lao aina ya Land Cruiser na kuelekea Mbagathi.

Lenzi za kamera za uchunguzi katika hospitali hiyo zilikuwa zikizunguka, zikichukua kila dakika moja kwa moja tangu kuwasili kwao hadi walipoondoka.

Picha zilionyesha polisi wakiwasili katika eneo la kuegesha magari la Hospitali ya Mbagathi saa 1:35 asubuhi Jumapili, Juni 8.

Ingawa kesi ya Ojwang' ilikuwa ya dharura, maafisa hao watatu walionekana kutokerwa na wakati baada ya kuteremka.

Picha ziliwaonyesha wakizunguka eneo hilo huku wakizungumza wao kwa wao, huku wakishirikisha simu zao kando.

Kisha walionekana wakifanya harakati za kwenda na kurudi hospitalini kabla ya kumpeleka Ojwang' kwenye mrengo wa dharura dakika 24 baadaye.

Video; hisani

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke