Albert Ojwang: Aliyehitilafiana na CCTV Akamatwa, Afichua Alilipwa KSh 3k

Katika hatua za mapema za uchunguzi wa mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang, IPOA ilibaini kuwa kamera za CCTV katika Kituo cha Polisi cha Central zilikarabatiwa kimakusudi

Kanda zilizobeba matukio yote yaliyopelekea kifo cha Ojwang katika kituo hicho zilifutwa kulingana na wataalam wa kuchunguza uhalifu wanaosaidia IPOA katika uchunguzi

Mtu anayeaminika kupewa kandarasi ya kutekelza uhalifu huo alikamatwa, na alipohojiwa, alifichua kuwa alilipwa KSh 3,000 kwa kazi hiyo

Mamlaka ya Kuchunguza Utendakazi wa Polisi (IPOA )imepata habari muhimu huku ikizidisha uchunguzi wake kuhusu mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang.

Inasemekana kuwa fundi alikiri kwa IPOA kukarabati CCTV iliyonasa matukio yote yaliyopelekea kifo cha mwanablogu Albert Ojwang katika Kituo cha Polisi cha Central Nairobi. Picha: NPS.

Chanzo: Twitter

Fundi aliyekuwa kwenye seli aliwafichuali wapelelezi kwamba alikarabti kamera za CCTV zilizonasa matukio yaliyosababisha kifo cha Ojwang katika Kituo cha Polisi cha Central.

Inasemekana alilipwa KSh 3,000 kufanya kazi iliyokusudiwa kuficha mauaji hayo kwa kufuta picha zote.

Alisema yeye sio mgeni katika kituo hicho, kwani mara nyingi amekuwa akiitwa kwa ajili ya kufanya ukarabati.

Fundi huyo aliwaambia wachunguzi kwamba aliitwa haraka kituoni Jumapili, Juni 8, saa chache baada ya Ojwang kuthibitishwa kufariki.

Alipofika, alitakiwa kufuta kanda za matukio katika kituo hicho kati ya Juni 6 na 8.

Aliwafichulia kwa maafisa wa hapo kwamba kufuta picha kwa siku maalum ilikuwa kazi isiyoweza kutenduliwa, na kwamba jambo la maana ni kuondoa yote yaliyomo kwenye Kinasa Video cha Dijiti (DVR), na hivyo kuvunja ushahidi ambao ungekuwa muhimu katika uchunguzi wa mauaji ya Ojwang.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke