Mchungaji Ng?ang?a Ataka Serikali Kuwakamata Vijana Wanaomkejeli Samia Suluhu: ?Peleka Kamiti?

Mwanzilishi wa kanisa la Neno Evangelism, Mchungaji James Ng?ang?a, hivi majuzi alisafiri hadi Marekani akiwa na mke wake mrembo

Mhubiri huyo amezungumzia vita vya mtandaoni kati ya Tanzania na Kenya, akionyesha kumuunga mkono Rais Samia Suluhu

Ng?ang?a ameitaka serikali kuwakamata Wakenya waliohusika katika kuunda picha za kejeli na matusi kumlenga Suluhu

Mchungaji James Ng?ang?a ameitaka serikali ya Kenya kuingilia kati kuhusu picha za AI zilizotengenezwa kumkejeli rais wa Tanzania, Samia Suluhu.

Mchungaji Ng?ang?a awakemea vijana wanaomdharau Samia Suluhu.

Chanzo: Instagram

Ng'ang'a alitoa maoni kuhusu mzozo wa mtandaoni kati ya Kenya na Tanzania, akimuunga mkono rais wa Tanzania.

Mhubiri huyo tata alisema vijana kuoka Kenya wamepotoka kwa kutumia picha na video zilizotengenezwa kwa teknolojia ya AI.

Mwanzilishi wa Neno Evangelism aliwakemea vijana wa Kenya waliobuni picha hizo, akisema ni dharau kwa rais wa kwanza mwanamke barani Afrika.

"Tumeenda Tanzania, mmemuweka mwanamke wa kwanza kuwa rais, mama wa kwanza Afrika kuwa rais, na mnamweka ndani ya jeneza. Mmefanya mbwa wazungumze, mkidai ni wanasiasa wa Kitanzania," alieleza.

Ng'ang'a alihimiza serikali ya Kenya kuingilia kati na kuwatia mbaroni waliohusika kutengeneza picha hizo.

Aliomba DCI kuwachukulia hatua vijana hao na hata kuwafunga miaka miwili.

"Serikali ya Kenya, tafadhali amkeni na mjaribu kuzima jambo hili. DCI, tafadhali kamata baadhi yao uwape adabu. Wachukue waende Kamiti kwa miaka miwili," alisema.

Nini kilitokea kati ya Kenya na Tanzania?

Mzozo wa mtandaoni kati ya Tanzania na Kenya ulizidi baada ya maafisa wa Tanzania kuwakamata na kuwarejesha kwa lazima wanaharakati wa Kenya.

Wanaharakati hao walijumuisha Boniface Mwangi na Martha Karua, waliokuwa wameenda Tanzania kuhudhuria kesi ya kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu.

Kabla ya kufukuzwa, wanaharakati hao walidaiwa kuzuiliwa bila mawasiliano kwa siku kadhaa, jambo lililowakasirisha Wakenya waliotuhumu Tanzania kwa kuvunja haki za kibinadamu.

Wabunge kutoka Tanzania walijibu kwa kuwakashifu Wakenya, wakisema wana "uelewa mdogo kiakili" na kuwatuhumu kwa kuingilia masuala ya Tanzania.

Hii ilisababisha ghadhabu kubwa mtandaoni ambapo Wakenya walipeleka jumbe nyingi kwa wabunge wa Tanzania na hata kutishia kususia muziki wa Bongo kama kisasi.

Je, Ruto aliomba msamaha kwa Tanzania?

Rais William Ruto alitoa msamaha wake wa dhati kwa rais wa Tanzania baada ya karibu wiki mbili za mabishano ya mtandaoni kati ya mataifa hayo mawili.

Ruto aliomba msamaha na kuelewana kwa pande zote mbili wakati wa hafla ya National Prayer Breakfast.

Aliwahimiza washirika wa kanda hiyo kuzingatia maendeleo na kujenga upya mahusiano huku wakiepuka makosa ya zamani.

Ujumbe wa rais ulionyesha dhamira ya kudumisha utulivu wa kikanda.

Kwa nini upinzani ulikataa msamaha wa Ruto?

Katika habari nyingine, vyama vya upinzani nchini Kenya vilitoa majibu makali kuhusu msamaha wa rais kwa umma.

Walimkemea rais kwa kushindwa kuwatetea Karua na Mwangi baada ya kufukuzwa kwao kwa utata.

Pia walidai haki kwa waathiriwa wa ukatili wa serikali na kutaka sheria zinazoathiri uhuru wa mtandaoni ziondolewe mara moja.

Taarifa hiyo ilisainiwa na vyama sita: People?s Liberation Party, Jubilee, Wiper, KANU, DAPK, na DP.

Walitoa taarifa hiyo mara tu baada ya rais kutoa hotuba yake.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke